Friday, May 18, 2012

MAITI INAYOTEMBEA (WALKING CORPSE)

Baada ya khojiwa na wale maafisa wa usalama, Precious (Shanice) alihakikishiwa kuwa wazazi wake watakuwa sawa kwa sababu tayari jitihada za kidiplomasia zilikuwa zikifanywa kati ya ubalozi wa Tanzania na serikali ya nchi hiyo. Kwa sababu kulikuwa na uhusiano mzuri wa kibalozi ati ya nchi hizo mbili, alihakikishiawa kuwa wazawi wake watakuwa salama na watarejea salama.

Taarifa ile ilikuwa njema sana kwa Precious (Shanice) na ilimuongezea nguvu za kupona haraka. Aliendelea kutibiwa ili kumaliza kabisa sumu ya madawa ya kulevya iliyokuwa ndani ya mwili wake. Wakati madaktari wakiendelea kumtibu, walibaini tatizo lingine.


Binti kabla ya kupata na tatizo hii ulikua unatumia kilevi gani?”
Akuu, mi situmii kilevi chochote.
“Hunywi pombe au kuvuta sigara?
“Wala, sijawahi hata siku moja.”
“Binti sema ukweli ili tukusaidie kwani tumebaini tatizo katika mfumo wako wa damu.”
“Dokta mbona unanilazimisha nikubali kitu ambacho sijawhai kukifanya?” aling’aka Shanice. Kwa kuwa daktari alikuwa mtu mzima na mwenye uzoefu wa kutosha kwenye fani yake ya utabibu, aliamua kutumia mbinu kali ili kupata ukweli kama Shanice alishakuwa ameanza kutumia madawa ya kulevya kabla ya siku ya tukio.

Alimtishia kuwa kuna dawa anataka kumpa lakini inatakiwa itumiwe na mtu ambaye hajawahi kunywa, pombe, kuvuta sigara au kutumia madawa yoyote ya kulevya. Akawambia kama alishawahi kufanya kimoja kati ya vitu hivyo, ni bora asema mapema kwani asiposema, endapo dawa ile ikianz kufanya kazi, uwezekano mkubwa ni kwamba atakufa.

“Unaniruhusu niendelee?” alisema daktari huu akivuta dawa kutoka kwenye kichupa kidogo kwa kutumia sindano. Maelezo yale yalimtisha sana Sahnice, ikabidi aseme ukweli.
“Dokta subiri kwanza, ukweli ni kwamba niliwahi kutuia madawa ya kulevya na kunywa pombe, naomba nibadilishie dawa nisije nikafa.”
Daktari alishusha pumzi ndefu baada ya kuupata ukweli.
“”Ilikuaje binti mdogo kama wewe uanze kujihusisha na mambo hatari kama matumizi ya dawa za kulevya?”
“Ni rafiki yangu alinishawishi.”
Wazazi wako wanajua?”
“Hapana hawajui chochote, nakuomba hata Mungu akiwasaidia wakarudi salama usiwaambnie kitu chochote,” alijitetea Shanice huku akigeukia ukutani kwa aibu. Daktari alimuahidi kuwa atamtunzia siri ilr lakini akaanza kwanza kumpa ushauri nasaha juu ya athari za madawa ya kulevya kwatika mwili wa binadamu. Alitumia muda mrefu kumuelewesha mpaka alipoona somo imemuingia kichwani.
“Niahidi kama hutarudia tena.”
“Nitajitahidi dokta lakini kuna muda mwingine nakuwa nashindwa kuvumilia.”
“Hiyo ni hali ya kawaida, itabidi uunganishwe katika tiba maalum iitwayo Rehabilitation na kwa sababu bado hayajakuathiri sana, uwezekano wa kupona ni mkubwa,” alisema daktari, wakakubaliana ambapo alimalizia kumpa dawa shanice kisha akamuacha apumzike.
***
Baada ya kukamatwa na polisi, Papaa Masafa akiwa njiani kupelekwa kituoni, aliendelea kuwashawishi wale polisi wakubaliane na ombi lake la kuuachilia huru kwa ahadi tamu kuwa atawalipa kiwango kikiubwa cha fedha kama shukrani. Licha ya awali kuonesha msimamo wa hali ya juu, wale polisi walianza kukonyezana na kupeana ishara juu ya nini cha kufanya baada ya kutangaziwa dau nono.

“Sikia broo, we twende kwanza kituoni tukaonekane kama tumetekeleza maagizo ya wakubwa wetu kisha mambo mengine yatafuatia,” alisema kiongozi wa msafara ule kwa sauti ya kunong’ona. Papaa Masafa aliomba kupea simu ili azungumze na vijana wake waliokuwa nchin Pakistan. Wale polisi walimruhusu, akaanza kuongea na upande wa pili wa simu.

 Kwa kuwa alikuwa akitumia lugha ya kiarabu, hakuna aliyeelewa. Akawa anawapa maeleezo vijana wake kuwa wanawake watatu ambao walikuwa tayari wameshauliwa na kupakiwa kiwango kikubwa cha madawa ya kulevya, wasafirishwe haraka kuja Tanzania lakini akaonya kuwa wasipitishwe kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na badala yake wapelekwe mpaka Lusaka< Zambia kisha wataingizwa nchini kwa kutumia barabara.

Aliwasisitiza kuwa Mzee Kibacha namkewe wasidhuriwe kwani tayari siri ilishafichuika nchini Tanzania. Upande wa pili ukamjibu kuwa hali ilikuwa mbaya zaidi kwao ka sababu wanajeshi wa Pakistan walikuwa wameizingira hospitali Balochistan Kashmir na kwamba uwezekano wa kutoroka ulikuwa mdogo.

“Tumieni njia ya handaki la chini ya ardhi kuwatorosha hao wengine ambao mmeshapaki mzigo kwenye miili yao vinginevyo mtakuwa mmesababisha hasara kubwa sana,” alisema kwa mamlaka kisha akakata simu. Taarifa kuwa hospitali yake nayo ilikuwa imezingirwa na polisi zilizidi kumchanganya Papaa Masafa, akawa anaongea peke yake kama mwendawazimu. Hakutaka kuamini kuwa mipango yake yote ingekwama kirahisi namna ile.


No comments:

Post a Comment